Tree Tv Online

UKURASA MAALUMU WA TAAARIFA NA HABARI MBALIMBALI TUNARAHISISHA TAARIFA KUFIKA KWENYE SOCIAL MEDIA KW

Photos from Tree Tv Online's post 08/02/2024

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (Bara) Ndg. Abdulrahman Kinana amesaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais wa Jamhuri ya Namibia Hayati Mheshimiwa Dkt. Hage G. Geingob. Ndg Kinana amesaini Kitabu hicho katika Ofisi za Ubalozi huo uliopo Masaki Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Februari, 2024.

Photos from Tree Tv Online's post 08/02/2024

MAKONDA AMTAKA AFISA ARDHI MAFINGA KUHAKIKISHA MWANAMAMA ALIYEDHULUMIWA NYUMBA YAKE NA MPENZI WAKE WA ZAMANI AMBAYE NI ASKARI ANAPATIWA HAKI YAKE*

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu. Paul Makonda amemtaka Afisa Ardhi wa Mafinga Mjini kushughulikia na kuhakikisha Mwanamama aliyetoa malalamiko ya kudhulimiwa nyumba yake na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani ambaye ni Askari aliyemtaja kwa jina la Mapunda.

Mara baada ya Mwanamama huyo kueleza malalamiko hayo, Mwenezi Makonda alimuuliza juu ya uwepo wa nyaraka za serikali ya hatimiliki ya nyumba hiyo ili kuthibitisha k**a ni yake kweli, Ambapo Mwanamama huyo alisema anazo hatimiliki hizp kuonesha uhalali wa umiliki wa nyumba hiyo.

Ndipo Mwenezi Makonda alipomuagiza Afisa Ardhi Mafinga Mjini kuzikagua na kujiridhisha juu ya nyaraka hizo.

Baada ya hayo yote, Makonda ametoa agizo la CCM la kuhakikisha Haki ya Mwanamama huyo haipotei.

📍Mafinga Mjini - Iringa
🗓️ 8 Februari, 2024

Photos from Tree Tv Online's post 08/02/2024

TEKNOLOJIA YA KISASA KUDHIBITI WANYAMA WAKALI NA WAHARIBIFU

Na Happiness Shayo- Dodoma

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) amesema Serikali itahakikisha inaendelea kutumia teknolojia ya kisasa kwa kadri inavyowezekana kudhibiti wanyama wakali na waharibifu hususan tembo ili kupunguza migogoro baina ya binadamu na wanyamapori.

Ameyasema hayo leo Februari 7,2024 katika kikao chake na Wabunge wa Mikoa ya Lindi na Mtwara kilicholenga kusikiliza changamoto wanazokabiliana nazo wananchi katika kuthibiti wanyamapori wakali na waharibifu katika maeneo yao kilichofanyika leo jijini Dodoma.

“Katika kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu hususan tembo tunatumia teknolojia ya Geofencing ambapo tutaweza kupata taarifa endapo tembo amesogea karibu na uzio uliowekwa na hivyo askari wetu watachukua hatua za haraka” Mhe. Kairuki amefafanua.

Pia, Waziri Kairuki amesema Serikali imeanza kutumia teknolojia ya kufukuza tembo kwa kutumia kamera za drones ambapo majaribio ya kwanza yamefanyika katika pori la Akiba la Selous.

Kuhusu uzio wa umeme amesema Serikali inaendelea na majaribio kuona k**a njia hiyo inafaa au la ambapo kwa sasa majaribio yamefanyika Pori la Akiba la Grumet.

Aidha, amewahakikishia Waheshimiwa Wabunge wa Mikoa ya Lindi na Mtwara kuwa Serikali inafanya kila liwezekanalo kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu katika maeneo yao.

“Niwahakikishie tutakapoweza kukodi helikopta tutafanya hivyo, itakapohitajika kutumia helikopta ya kwetu tutafanya lakini kwa sasa tunaangalia tufanye nini kwa kudhibiti wanyama hao kwa kutumia mikakati ya muda mfupi na ya muda mrefu”amesisitiza Mhe. Kairuki.

Amesema pia Serikali inafanyia kazi madai ya kifuta jasho na kifuta machozi ambapo mpaka sasa uhakiki umeshafanyika hivyo ufuatiliaji wa fedha unaendelea ili wahusika walipwe.

Kuhusu kutangaza vivutio vya utalii vya ukanda wa kusini, Mhe. Kairuki amesema Serikali itafanya tathmini ya kina kuweza kuviibua, kuvitangaza na kuviendeleza vivutio vya utalii vya Ukanda wa Kusini hasa Kilwa Kisiwani na maeneo ya fukwe ya Pangani, Mkinga na Mafia.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Mhe. Salma Kikwete amesema maeneo mengi ya Mikoa ya Lindi na Mt

Photos from Tree Tv Online's post 06/02/2024

OMAN NA TANZANIA ZAKABIDHIANA VIFAA VYA UHIFADHI WA MIKUSANYO YA KIMAKUMBUSHO

Na Happiness Shayo- Dar es Salaam

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) ameshuhudia makabidhiano ya vifaa vya awali kati ya Makumbusho ya Taifa la Tanzania na Makumbusho ya Sultani ya Oman, vitakavyotumika kwa ajili ya kuhifadhia mikusanyo mbalimbali iliyopo katika Makumbusho ya Tanzania.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo tarehe 6 Februari 2024 katika Kituo cha Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni kilichopo Posta jijini Dar es Salaam.

Awali, akizungumza na Ujumbe wa Wataalamu kutoka Makumbusho ya Sultani ya Oman na Makumbusho ya Taifa la Tanzania, Mhe. Kairuki ameushukuru ujumbe huo kwa kuweza kuleta baadhi ya vifaa vya awali ikiwa ni mwanzo mzuri wa kutekeleza Mkataba wa Mashirikiano baina ya Makumbusho ya Taifa la Tanzania na Makumbusho ya Sultani ya Oman.

Kufuatia hatua hiyo, Mhe. Kairuki ameahidi pamoja na mambo mengine kuvionyesha baadhi ya vifaa vya kiutamaduni vya Sultani ya Oman katika Makumbusho ya Taifa la Tanzania ili watu waweze kujua na kujifunza utamaduni wa Oman.

Aidha, Mhe. Kairuki ametumia fursa hiyo kumshukuru Mtendaji Mkuu wa Makumbusho ya Sultani ya Oman, Mhe. Jamal bin Hassan Al Moosawi kwa kukubali ombi maalum la ujenzi wa jengo litakalokuwa Kituo cha Kiutamaduni cha Kiswahili na Oman.

Waziri Kairuki ametoa wito kwa wataalamu wa pande zote mbili za Tanzania na Oman kuweka juhudi katika kuratibu mradi huo vizuri na kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa la Tanzania, Dkt. Noel Lwoga amesema kikao hicho kimejikita katika kuainisha maeneo ya kuweka mradi wa jengo la kiutamaduni la Kiswahili na Oman, kupitia eneo ambalo litakwenda kuboresha Onesho la Historia nchini, kupitia mikusanyo yote ambayo ina viashiria vya mashirikiano baina ya Oman na Tanzania ili kuviainisha vinahitaji uhifadhi wa aina gani, vinaweza vikaoneshwa namna gani kule Oman na nchini Tanzania.

Tanzania na Oman zilisaini Mkataba wa Makubaliano (MOU) Juni 13, 2022 na baada ya majadiliano ya muda mrefu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki iliwezesha kufanyika kwa mkutano wa kwanza wa pamoja baina ya Mak

Photos from Tree Tv Online's post 06/02/2024

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu. Paul Makonda amekemea vikali tabia ya baadhi ya Viongozi walioaminiwa na kupewa Wizara na matokeo yake kutofanya kazi kwa kumsadia Rais Samia badala yake wanatengeneza makundi ya watu kuwasifia na kusababisha uzembe kufanyika kwa watendaji wa ngazi ya chini hali inayopelekea Wananchi kutohudumiwa na kutopata maendeleo kwa wakati.

"Mimi wala sihitaji Viongozi wa Serikali wasiofanya kazi wanipende kwa madudu yao, ziara hizi tunazofanya CCM titaeeka bayana kila sekta ili kuona kazi inafanyika au laa wapo baadhi ya Viongozi wengine wameaminiwa na kupewa Wizara badala ya kufanya kazi walizopewa wao wanahangaika kutnegeneza watu wa kuwasifia badala ya kuwasimamia watendaji wao huku chini maana mambo hayaendi vema sehemu nyingi"

"Uzuri ni kwamba mimi siogopo kuchukiwa wala kusemwa na bahati mbaya mimi sio muoga yani siogopi chocjote na nimeapa sitamdanganya Mwenyekiti wetu wa CCM na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan , lazima nimwambie ukweli sehemu yoyote nikikuta madudu yoyote"

"Mwenyekiti wa CCM na Rais Dkt. Samia ametoa fedha nyingi saba kwa miradi mbalimbali ya maendeleo nchi nzima katika kila Wizara kila Sekta lakini baadhi ya Viongozi hawasimamii kwa kufuatilia na matokeo yake wanampelekea taarifa Mhe. Rais kwamba mambo yapo sawa kumne chini huku Wananchi wanateseka , hilo kwangu kupitia ziara hizi sitalifumbia macho"

Mwenezi Makonda ameyasema hayo wakati akisalimiana na kuzungumza na Wananchi wa Mji mdogo wa Laela akiwa njian kuelekea Mkoani Songwe kwa muendelezo wa ziara yake ya Mikoa 20 Back To Back.

📍Mji mdogo wa Laela - Rukwa
🗓️ 6 Februari, 2024

Photos from Tree Tv Online's post 06/02/2024

"FTI NI CHUO BORA DUNIANI” WAZIRI KAIRUKI

Na Happiness Shayo

Chuo cha Misitu Olmotonyi (FTI) ni chuo pekee kikubwa tangu kuanzishwa kwake mwaka 1937 na ni moja ya chuo bora kabisa kuwepo Afrika Mashariki, Afrika na Duniani, katika utoaji wa mafunzo ya misitu kwa nadharia na vitendo.

Hayo yamesemwa leo Februari 5,2024 na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) alipofanya ziara ya kikazi katika chuo hicho kilichopo jijini Arusha.

Chuo hicho kimekuwa kikitoa mafunzo ya misitu katika kozi za Astashahada ya awali ya misitu, Astashahada ya Misitu, Stashahada ya Misitu, Stashahada ya Misitu ya mijini na usanifu wa mandhari, stashahada ya jioinfomantiki katika usimamizi wa maliasili (Geoinformatics for Natural Resources and Management) pamoja na mafunzo ya muda mfupi ya misitu na uhifadhi wa mazingira.

Waziri Kairuki amesema ili kukikuza zaidi chuo hicho, Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii inaendelea kufanya mapitio ya mitaala yake kuhakikisha kwamba inaendana na mahitaji ya sasa ya kidunia katika taaluma ya ulinzi, usimamizi na uendelezaji wa misitu.

Aidha, amesema Wizara itaendelea kuboresha mazingira ya chuo hicho ikiwa ni pamoja na kuangalia namna ya kuongeza karakana, mashine mpya, majengo mapya na maboresho mengine.

“Tunaweka mkazo kuhakikisha kwamba tunaboresha miundombinu ili tuweze kuwa na wanafunzi wengi zaidi, wataalamu wa ndani watakaoenda kufanya kazi katika kulinda na kuendeleza misitu yetu ikizingatiwa kwamba Tanzania ina eneo kubwa sana la misitu inayosimamiwa na Serikali Kuu, Serikali za mitaa kupitia vijiji na watu binafsi hasa tukitambua umuhimu wa misitu yetu katika utunzaji wa mazingira, uwepo wa vyanzo vya maji na masuala mengine kwa ujumla wake” Mhe. Kairuki amesisitiza.

Awali, akizungumza na menejimenti ya chuo hicho , Waziri Kairuki ameitaka kuendelea kukitangaza zaidi chuo hicho.

“Tuendelee kukitangaza chuo kwa kadri inavyowezekana na tujiimarishe zaidi katika utoaji wa mafunzo haya ili tuvutie wataalamu kutoka ndani na nje ya nchi” amesema Mhe. Kairuki.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Misitu Olmotonyi,Dkt. Joseph Makero ameahidi kuwa watumishi wa chuo hicho wanajitahidi kufanya majukumu yao.

Photos from Tree Tv Online's post 06/02/2024

📍 JIMBONI TEMEKE.
Mhe Dorothy George Kilave Mbunge wa Jimbo la Temeke amefika Mtaa wa Mzambarauni, kuzungumza na Wananchi katika Ziara ya kawaida.

Katika Ziara hii ya matembezi ya kawaida, Mhe Mbunge alikutana na Viongozi wa CCM Tawi la Mzambarauni, Kisha aliambatana na Mkt wa Mtaa, Kwa Pamoja
Walielekea Mtaani kuonana na Wananchi na Kuzungumza nao.

Pia, Mhe Mbunge alitumia Wakati huo, kuwajulia hali Baadhi ya Wazee Wanaoishi Mtaa wa Mzambarauni wenye Changamoto za kiafya.

Kwa Pamoja, Wananchi wamewasilisha Kero Mbalimbali ambazo bado zinawakabili, Pamoja na kuishukuru Serikali ya Awamu ya Sita Chini ya *Dkt Samia Suluhu Hassan* kwa Miradi ya Afya (Kituo cha Afya) na Elimu (Majengo ya Ghorofa Lumo Sekondari) NK, iliyoendelezwa Ndani ya Kata ya Yombovituka.

Kisha, Wananchi wamewasilisha Hitaji kubwa la maboresho ya Baadhi ya Barabara, Pamoja na Kusambazwa Maji ya DAWASA katika Kaya Ndani ya kata.

Mhe Mbunge, Amesema Changamoto hizo Alisha zifikisha katika Mamlaka husika pia Ameahidi kuwa Serikali inaendelea Kuzifanyia kazi, ili kuhakikisha inaboresha Mahitaji ya Wananchi.

Mhe Dorothy Kilave Kwa Maendeleo ya Jimbo la Temeke.

04/02/2024

"Rais (Samia Suluhu Hassan) alisema yawezekana wana jambo (CHADEMA) tuwasikilize; huo ni uungwana. Ukaanzishwa mchakato mwingine maalum wa kuwasikiliza ndugu zetu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo."

"Hoja zote tulizozijadili kwa mwaka mzima katika vikao 11 ni hoja zilizotokana na CHADEMA hakuna hoja hata moja ya CCM. Ni uungwana gani unaotaka zaidi ya hapo?"

"Rais (Samia Suluhu Hassan) aliagiza Serikali itafute utaratibu wa kuwalipa (CHADEMA) madai ya ruzuku. Wakalipwa shilingi bilioni 2.7; madai yao ya tangu uchaguzi ulipokwisha."

"Tarehe 03 Desemba 2023 pale Ikulu Dar Es Salaam, aliitisha kikao (Rais Samia Suluhu Hassan) ikaruhusiwa mikutano ya hadhara. Wakaanza (CHADEMA) kumvaa Rais na kuanza kutoa maneno ya kejeli na dharau."

" wananchi hawataki kusikia dharau, hawataki kusikia kashfa, wananchi hawataki matusi "

Komredi Abdulrahman Kinana, Ukumbi wa Diamond Jubilee - Dar Es Salaam.

Mkutano wa Wanachama na Viongozi wa Mkoa wa Dar Es Salaam, 04 February 2024.

Photos from Tree Tv Online's post 04/02/2024

"Mchakato wa katiba kwenye nchi yeyote sio wa mwaka mmoja. Kuna mageuzi madogo kwenye katiba, kuna sheria zimepelekwa Bungeni; sheria ya Uchaguzi wa Madiwani, Wabunge na Rais, sheria ya Tume ya Uchaguzi na mabadiliko ya sheria ya vyama vya siasa, lengo lake ni kuboresha uchaguzi wa mwaka 2024 na 2025."

"Uchaguzi sio tume tu, uchaguzi ni sera, kujipanga, kujieleza, kusikiliza watu pamoja na kuwa na muundo mzuri wa uchaguzi ndani ya Chama chako."

Komredi Abdulrahman Kinana, Ukumbi wa Diamond Jubilee - Dar Es Salaam.

Mkutano wa Wanachama na Viongozi wa Mkoa wa Dar Es Salaam, 04 February 2024.

Photos from Tree Tv Online's post 04/02/2024

"Maridhiano sio ya vyama tu (vyama vya siasa) bali maridhiano ni ya jamii kwa ujumla katika kujenga umoja na mshik**ano wa taifa letu."

"Chimbuko la maridhiano lilianza tarehe 24 Aprili 2021. Maridhiano yana pacha wake, pacha wake ni ustahimilivu. Hakuna maridhiano bila ustahimilivu."

"Katika vikao vyote; (Baraza la Vyama, Kituo cha Demokrasia) ndugu zetu CHADEMA hawakushiriki, hawakutaka kwenda. Kikaundwa kikosi kazi hawakwenda, wengine wote walienda lakini wao hawakwenda."

"Hoja zote tulizozijadili kwa mwaka mzima katika vikao 11 ni hoja zilizotokana na CHADEMA hakuna hoja hata moja ya CCM. Ni uungwana gani unaotaka zaidi ya hapo?"

Komredi Abdulrahman Kinana, Ukumbi wa Diamond Jubilee - Dar Es Salaam.

Mkutano wa Wanachama na Viongozi wa Mkoa wa Dar Es Salaam, 04 February 2024

Photos from Tree Tv Online's post 04/02/2024

"Hiki Chama kikubwa (CCM), kinaheshimika, kinapendwa na kimepewa nafasi ya kuongoza kwa sababu ya sera nzuri."

"Ukweli usiposemwa na upotoshaji ukaendelea, upotoshaji unageuka kuwa ukweli na hilo hatulikubali."

"Siku zote Chama Cha Mapinduzi kimekuwa na dhamira, nia na makusudio mema kwa watanzania."

Komredi Abdulrahman Kinana, Ukumbi wa Diamond Jubilee - Dar Es Salaam.

Mkutano wa Wanachama na Viongozi wa Mkoa wa Dar Es Salaam, 04 February 2024.

04/02/2024

📌 Bado Siku 1 kuelekea maadhimisho ya Siku ya Usalama Mtandaoni; tarehe 6 Februari 2024.📌

Kaulimbiu: ”Unavutiwa na mabadiliko mtandaoni? Fanya tofauti na ongoza ushawishi”

Photos from Tree Tv Online's post 04/02/2024

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa amewaelekeza Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanasimamia matumizi ya magari mapya 13 yaliyotolewa na Serikali kuwa yanaleta tija ya kuwahudumia watumishi na wananchi.

Mheshiwa Mchengerwa aliyasema hayo hapo jana tarehe 03 Februari, 2024 wakati akifungua kikao kazi cha kushughulikia changamoto za upandishaji wa vyeo na kubadilisha kada kwa walimu katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

Mheshimiwa Mchengerwa pia amewataka viongozi hao kote nchini kuhakikisha katika taarifa zao za utendaji kazi wa kila mwezi anapata taarifa ya utendaji kazi wa Maafisa Elimu na Idara ya Afya ili kuona k**a magari yaliyotolewa kwa shughuli za ufuatiliaji na utatuzi wa kero za wananchi zinafanyiwa kazi kwa wakati pamoja na Maafisa Elimu kwenda vijijini kutatua kero za walimu.

“Maafisa Elimu fanyeni mikutano na walimu, nendeni mshuke vijijini mkatatue kero na changamotoa za walimu mara moja na zile zilizo nje ya uwezo wenu kazileteni kwetu” Alisema Mheshimiwa Mchengerwa.

Waziri Mchengerwa alifanya zoezi la kugawa magari 13 yenye thamani ya Zaidi ya Shilingi Bilioni 1.8 yatakayosaidia ufuatiliaji wa masuala ya elimu msingi katika Halmashauri 13 kupitia Mradi wa Kukuza Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (GPE LANES II) na kuwaelekeza viongozi wa Mikoa na Wilaya kufuatilia matumizi sahihi ya magari hayo.

Katika hatua nyingine Waziri Mchengerwa alisema Serikali ilisaini Mradi mpya na Wadau wa GPE ambao una afua za kutatua changamoto za walimu nchini unaojulikana k**a ‘Teacher Support Programme’ (TSP) wenye thamani ya shilingi Bilioni 264 ambao umeanza katika mwaka wa 2023/2024 ikiwa ni matunda ya Mheshiwa Dkt. Rais Samia Suluhu Hassan ambaye anaimarisha mahusiano ya kimataifa na nchi na Wadau mbalimbali wa maendeleo.

Awali Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Serikali za Mitaa Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo alisema magari yaliyotolewa na Programu ya Kuimarisha Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (GPE LANES II) yatasaidia kuhamasisha utendaji kazi na utekelezaji wa kitaaluma hasa maeneo ya pembezoni kwani yatasaidia kuongeza kiwango cha ufaulo.

Photos from Tree Tv Online's post 04/02/2024

Waziri wa Nchi, Mhe. Mohamed Mchengerwa amefungua kikao kazi cha Maofisa Utumishi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali wanaohakiki kwa kina changamoto za walimu hususan upandishwaji wa vyeo.

Akifungua leo Februari 3, 2024 kikao hicho jijini Dodoma, Waziri Mchengerwa amesema katika kuhakikisha kuwa malalamiko ya Walimu yanashughulikiwa, Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais UTUMISHI iliagiza Tume ya Utumishi wa Walimu kufanya uchambuzi na kubaini walimu wote wenye changamoto katika upandaji wao wa vyeo.

"Niwapongeze Watendaji wa Tume ya Utumishi wa Walimu kwa kazi nzuri ambayo wameifanya ambapo uchambuzi umefanyika na walimu zaidi ya 136,000 wamebainishwa kuwa na changamoto,
pamoja na kazi nzuri iliyofanyika, kwa kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa malalamiko ya walimu wote yanashughulikiwa kwa ufanisi, nimeelekeza uhakiki wa kina ufanyike kwa kuhusisha taarifa za watumishi k**a zilivyo kwenye Mfumo wa Taarifa za kiutumishi na Mishahara (HCMIS)," amesema

Ameagiza kushughulikia kikamilifu changamoto hizo ndani ya siku 14 na kufanya kazi hiyo kwa ufanisi wa hali ya juu ili kuhakikisha hakuna Mwalimu anayeachwa baada ya zoezi hilo kufanyika.

Wakati huohuo, Waziri Mchengerwa amewakumbusha Waajiri na Mamlaka zote zinazohudumia Walimu kusimamia vyema maslahi ya walimu ikiwa ni pamoja na kutatua kero walizo nazo.

"Naomba niweke wazi mimi sitamvumilia mtendaji yeyote ambaye hawajibiki kushughulikia kero za walimu na vilevile sitamani kusikia walimu wana malalamiko kuhusu maslahi yao ya kiutumishi,"amesema.

Photos from Tree Tv Online's post 03/02/2024

Huduma zote za Mahak**a Kuu-Masjala Kuu zilizokuwa zikitolewa Dar es Salaam, zimehamishiwa Dodoma* katika jengo jipya la Makao Makuu ya Mahak**a ya Tanzania (Judiciary Square) lililopo Dodoma mtaa wa Mahak**a eneo la Tambukareli kuanzia tarehe 30 Januari, 2024.

Photos from Tree Tv Online's post 03/02/2024

📍 Kuelekea Maadhimisho ya Miaka 47 ya CCM.

Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Temeke imeadhimisha Miaka ya 47 ya CCM Kwa kufanya Usafi katika Eneo la Ofisi za CCM Wilaya ya Temeke , Sanjari na Hilo, Jumuiya ya Wazazi kupitia Mwenyekiti wake Ndugu Slim, aliyeambatana na Ndugu Laurent Mganga Katibu wa Elimu na Malezi Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dar es salaam, Kwa Niaba ya *Mhe Dorothy George Kilave* Mbunge wa Jimbo la Temeke wamekabidhi Vitabu Vya Sayansi Kwa ajili ya Shule za Sekondari Jimboni Temeke.

Hafla ya Makabidhiano imefanyika katika Shule ya Sekondari Kibasila na Imehudhuriwa na Ofisi ya Mbunge Temeke, Dr Balongo Afisa Elimu Sekondari, Manispaa ya Temeke na Baadhi ya walimu wa Shule Sekondari Jimboni Temeke.

Kwa Ujumla, Viongozi wa CCM kupitia Jumuiya ya Wazazi wamepongeza Jitihada za Mhe Mbunge katika kuunga Mkono Maendeleo ya Elimu Jimboni Temeke.

Mhe Dorothy Kilave Kwa Maendeleo Jimbo la Temeke.

Kauli Mbiu, *"Miaka 47 ya CCM, shiriki Uchaguzi Kwa Uadirifu,kazi iendelee "*

Photos from Tree Tv Online's post 03/02/2024

Washiriki wa Shindano la Tano la Usalama Mtandaoni (Cyber Champions)2023/24 linaloratibiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), wakiwa katika fainali za shindano lililofanyika katika Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu- Chuo Kikuu cha Dodoma (CIVE-UDOM), tarehe 2 Februari, 2024.

Washiriki 50 kutoka taasisi mbalimbali za Elimu ya Juu wameshiriki Shindano hilo lililoandaliwa kwa lengo la kuibua na kukuza uwezo kwa vijana, kuimarisha na kukabili vihatarishi vya usalama mtandaoni.

Photos from Tree Tv Online's post 03/02/2024

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt Jabiri Bakari katika picha ya pamoja na washiriki na watoa mada wa Usalama Mtandaoni, iliyofanyika katika Ofisi za Makao Makuu , TCRA Dar Es Salaam Ijumaa, tarehe 2 Februari 2024.

Semina hii ni sehemu ya shughuli zilizoandaliwa kuelekea maadhimisho ya siku ya Usalama Mtandaoni, itakayofanyika tarehe 6 Februari 2024.

Photos from Tree Tv Online's post 03/02/2024

Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA Dkt. Jabiri Bakari akizungumza na washiriki wa semina ya Usalama Mtandaoni, iliyofanyika katika Ofisi za Makao Makuu , TCRA Dar Es Salaam Ijumaa, tarehe 2 Februari 2024.

Katika semina hiyo Dkt Bakari amesema elimu endelevu ya usalama mtandaoni ni muhimu ili kufanya teknolojia iwe na tija kwa wananchi.

Semina hiyo imewahusisha Umoja wa madereva Bodaboda na umoja wa wajasiriamali wanawake.

Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Usalama Mtandaoni hufanyika kila jumanne ya pili ya mwezi Februari kila mwaka ambapo mwaka huu itakuwa Februari 6.

Photos from Tree Tv Online's post 02/02/2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bi. Doris Ntuli Kalasa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino leo siku ya tarehe 02.02.2024

Bi. Doris Kalasa anachukua nafasi ya Masanja Robert aliyekuwa katibu tawala wa mkoa huo ambaye muda wake wa kustaafu ulifika.

Photos from Tree Tv Online's post 02/02/2024

📌TAARIFA KWA UMMA📌

02/02/2024

📌 Bado Siku 3 kuelekea maadhimisho ya Siku ya Usalama Mtandaoni; tarehe 6 Februari 2024.📌

Kaulimbiu: ”Unavutiwa na mabadiliko mtandaoni? Fanya tofauti na ongoza ushawishi"

Photos from Tree Tv Online's post 02/02/2024
Photos from Tree Tv Online's post 02/02/2024

📍IRINGA

Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Ikiongozwa na Mwenyekiti wake Ndugu. Mary Chatanda (MCC) imeendelea kusimama kidete katika kuhakikisha inamsaidia Mwanamama Maria Ngoda ambapo jan Tarehe 01 Februari, 2024, Mahak**a Kuu ya Mkoa Wa iringa Chini ya Jaji Mfawidhi Mgetta imesikiliza kesi ya Rufaa Namba 84101/2023 kati ya Ndg Maria Ngoda (almaarufu Mama wa Nyama wa Swala) Dhidi ya Jamhuri.

Akiongoza jopo la Mawakili nane (8) upande wa mrufani wakili Moses Ambwindile wakishirikiana na Mwanasheria Kutoka Umoja wa wanawake (UWT) Amesema, wametetea Sababu zao za Rufaa 14 mbele ya Jaji Mfawidhi , Aidha Jaji Mgetta ameahirisha Shauri hilo mpaka hapo tarehe 2 Februari, 2024 (leo).

Mfungwa Maria Ngoda (mkata rufaa) alihukumiwa kifungo cha miaka 22 kwa kukutwa na vipande 12 vya nyama ya swala mnamo tarehe 3 Novemba, 2023.

Photos from Tree Tv Online's post 02/02/2024

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Dkt. Balozi Emmanuel John Nchimbi na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Ndugu Nape Moses Nnauye, ambaye pia ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, wakiwa wamezama kwenye mazungumzo mazito kuhusu masuala mbalimbali, baada ya Waziri huyo kumtembelea Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Nchimbi ofisini kwake, Makao Makuu ya CCM, jijini Dodoma, Alhamis, Februari 1, 2024.

Photos from Tree Tv Online's post 02/02/2024

📌 Bado Siku 4 kuelekea maadhimisho ya Siku ya Usalama Mtandaoni; tarehe 6 Februari 2024.📌

Kaulimbiu: ”Unavutiwa na mabadiliko mtandaoni? Fanya tofauti na ongoza ushawishi"

Photos from Tree Tv Online's post 31/01/2024

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. (Mb) akijadiliana jambo na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi (Mb) katika kikao cha pili Mkutano wa 14 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma leo Januari 31,2024.

Photos from Tree Tv Online's post 31/01/2024

Wadau wa sekta mipango miji wamekutana Jijini Dodoma kujadili rasimu ya marekebisho ya Kanuni za Sheria za Mipango Miji nchini ili ziendane na mabadiliko ya kasi ya ukuaji miji pamoja mchango wake wa sekta hiyo katika hafua muhimu za kuifadhi mazingira.

Akifungua kikao hicho Januari 30, 2024 jijini Dodoma, Naibu Katibu Wizara ya ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi Lucy Kabyemera amesema kuwa ardhi inahitaji kupangwa, kupimwa, kumilikishwa na kuendelezwa ikiwa katika hali nzuri kiuchumi, kijamii na kimazingira.

“Natambua ili kufanikisha azma hii, tunahitaji kuwa na kanuni sahihi za kuongoza upangaji wa miji yetu pamoja na matumizi mbalimbali ya ardhi hapa nchini” Naibu Katibu Bi Kabyemera.

Upangaji miji unaongozwa na Sheria ya Mipango Miji sura Na. 355 na Kanuni zake za mwaka 2018 ambazo zinahitaji kuboreshwa kutokana na mabadiliko ya kiuchumi, kimazingira, mitazamo ya kimaisha, kimaendeleo pamoja na mitazamo ya kimataifa vimekuwa msingi wa kupitia upya kanuni hizo ili ziendane na hali ya sasa.

Wadau hao ni pamoja na Manejimenti ya Wizara, Makamishna wa Ardhi Wasaidizi kutoka mikoa ya Tanzania Bara, wawakilishi kutoka Wizara mbalimbali, taasisi za Serikali pamoja na zisizo za Serikali.

Want your business to be the top-listed Media Company in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Videos (show all)

Tembelea "Tanzanite Portal" kwenye ukurasa wa tovuti ya TCRA:  www.tcra.go.tz ili kujisajili na kutuma maombi yako ya le...
Makonda aingia Simiyu na mkokoteni unaovutwa na Punda. #ZiaraYaMwenezi
RAIS DK.MWINYI ASEMA ELIMU NI KIPAUMBELE KIKUBWA CHA SERIKALI. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk....
📌Maana ya Klabu za Kidijiti au Digital Clubs📌#tcratz #digitalclubs #klabuzakidijiti #stem #digitalclubstanzania
Shabiki wa @simbasctanzania Leo siku ngumu kwao Shabiki wa @yangasc unashangilia kutokea wap#KariakooDerby
NANSIO - UKEREWEMkuu wa wilaya Ukerewe Mhe. Hassan Bomboko ameshiriki mkutano mkuu wa vyombo vya watoaji huduma ya maji ...
MAKONDA KUANZA ZIARA YA MAFUNZO NA ITIKADI YA CCM PAMOJA NA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO - KANDA YA ZIWAKatibu wa Halmasha...
UMEMSHUKURU MUNGUJumapili Leo sema neno la kumshukuru Mungu Usiwaze matatizo yako Usiwaze magumu yako Kaza yatasogea.......
📍BASHUNGWA AWAPA MENO BODI MPYA YA USHAURI YA TANROADS"Nendeni Mkaokoe Mabilioni ya Watanzania, Mkague Miradi ya Barabar...
MWANZA -MWANZAMkuu wa wilaya Ukerewe Mhe. Hassan Bomboko amemuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla  ka...
Rais Samia ashiriki Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika (SADC) Lua...
Kila mtumiaji wa huduma za mtandao anapaswa kutimiza jukumu lake kuhakikisha usalama mtandaoni unadumishwa.#tcratz #elim...

Telephone

Website

Address

Tabata
Dar Es Salaam
Other Media/News Companies in Dar es Salaam (show all)
Media in Motion Ltd. Media in Motion Ltd.
Dar Es Salaam

• Video/TV • Music • Web Development • Photography

Mwananchi Mwananchi
Mwananchi
Dar Es Salaam, 19754

Gazeti namba #1 la Kiswahili Tanzania. Web: www.mwananchi.co.tz FB: https://www.facebook.com/MwananchiNews Twitter: https://twitter.com/MwananchiNews

antomatv antomatv
Musoma
Dar Es Salaam

Official Antomatv Online page | LIKE FOLLOW SHARE | Call 0759 891 849 - 0653 266 834

Hot news To day Hot news To day
Wiloles
Dar Es Salaam, HOUSE

Habari Mpya Media Habari Mpya Media
Www. Habarimpyamedia. Blogspot. Com
Dar Es Salaam

Elishadai One_Media Elishadai One_Media
TABATA
Dar Es Salaam

Mzunguko Online Mzunguko Online
Mkwajuni, CCM Makongo Juu
Dar Es Salaam, 255

Kabeta Mkapa Kabeta Mkapa
Keko Juu, Temeke
Dar Es Salaam

news & updates

CB online Tv CB online Tv
Dar Es Salaam

welcome to CB online TV Page Official page The Home of Entertainment News, Music, Politics

YANGA News YANGA News
Dar Es Salaam

official page for all news apdated to our club

Big Bros Media Big Bros Media
Namanga
Dar Es Salaam, 14111

📻 Welcome to Big Boss Radio, where the heartbeats of Tanzania unite! 🇹🇿🎵 #BigBossRadio

Kipe style ent Kipe style ent
Gongo La Mboto
Dar Es Salaam

sanaa kazi tuitunze itutunze na kutupa heshima