Wisdom&Wellness Meditation Garden
Love Yourself Simple ... self-care with the simplest ingredients in nature! We promote health & well
Tabia ya mtu inaendana na uwezo alionao kwa wakati au majira anayopitia. Mwenyezi Mungu amemjalia kila mtu tabia ambayo haifanani na mtu mwingine....
Kidole ni sehemu katika mwili wa binadamu ambacho kipo mguuni na mkononi. Ulimi ni sehemu ndogo ambayo ipo ndani ya mdomo. Unaweza kujikwaa kidole kilichopo mguuni wakati unatembea kwa kujigonga kwenye jiwe au kwenye sehemu yoyote iliyo ngumu. Ukijigonga, unaweza kuumia na hata kutoka damu. Utakachoweza kufanya ni kusafisha ile damu na ikibidi ukaenda hospitali kutibiwa....
Maskini ni mtu asiyejiweza. Umaskini ni kitu kibaya sana kwa jinsi watu wanavyouchukulia. Umaskini unanyanyapaliwa na wengi katika jamii. Mtu hazaliwi maskini kwa sababu amependa. Hujikuta amezaliwa hivyo....
Katika kijiji kimoja alikuwepo mfanya biashara mmoja aliyekuwa akiuza siagi. Mfanya biashara huyu alikuwa na mteja wake maalum mjini ambaye alikuwa na duka kubwa la vyakula. Hawa wawili walikuwa na makubaliano ya kubadilishana bidhaa. Makubaliano hayo yalikuwa hivi: siagi katika vifungashio vya kilo moja moja,kwa bidhaa za vyakula tofauti tofauti. Kwa maana hiyo, wafanya biashara hawa wawili walikuwa hawauziani bali wanabadilishana kufuatana na makubaliano yao....
Maneno ni matamshi yaliyoandikwa ama yaliyotamkwa kutoka kwenye vinywa vya watu. Mathalani, maneno yanaposemwa juu yako ni budi ukayatafakari kwanza ili ujue yana maana gani. Endapo maneno hayo hayaleti madhara yoyote basi hayatakuwa na shida kwako, shida itakuwa pale tu mtu atakapokushikia silaha na akakudhuru....
Mcheza kwao ni mtu ambaye anajishughulisha sana na mambo yanayofanyika kwenye jumuiya yake. Kutunzwa ni kupewa tuzo/zawadi pale atakapofanikisha jambo. Kiubinadamu huwa ni jambo zuri kutambuliwa mchango wao pale mtu afanyapo vizuri, iwe ni kwenye jumuia, masomo, kilimo ama eneo la kazi. Hata katika familia, inatakiwa zawadi zitolewe kwa wana familia....
Samaki ni kiumbe kinachoishi majini. Mara baada ya kuvuliwa, baadhi ya samaki hutakiwa kukunjwa kwa ajili ya kuhifadhiwa au kwa matumizi ya baadaye. Ili huo mchakato uende vizuri ni lazima samaki hao wakunjwe kulingana na mahitaji ya mlaji. Endapo samaki atakawizwa kukunjwa mara baada ya kuvuliwa, huharibika kiasi kwamba hataweza kukunijka tena....
Tembo ni mnyama mkubwa kuliko wote waishio porini. Kwa upande mwingine, sisimizi ni mdudu mdogo sana kiasi kwamba usipoangalia kwa makini, unaweza usimuone kwa jinsi alivyo mdogo....
Adui ni mwanadamu ambaye hayupo katika upande wa mwanadamu mwenzake yaani asiyekuwa na upendo kwa mwenzie. Njaa ni hali ya kukosa chakula. Sote tunajua kuwa mahitaji muhimu kwa mwanadamu ni chakula, mavazi na mahali pa kuishi. Mavazi na mahali pa kuishi sio muhimu sana ukilinganisha na mahitaji ya chakula kwa sababu bila chakula mtu hawezi kuishi....
Maisha ya mwanadamu yamegawanyika katika maeneo mbalimbali na tofauti. Kipindi cha mpito hakina budi kutokea kwa kila mtu. Hakuna ambaye anaweza kusema hajapitia nyakati ngumu katika maisha yake. Kuna nyakati nyingine unapitia magumu kwa ajili ya kukuvusha na kukupeleka mahali fulani....
Kwa kawaida kuna mashindano ya aina mbali mbali katika nyanja tofauti tofauti kulingana na mazingira ya sehemu husika. Mtu yeyote anapoingia kwenye mashindano yoyote yale hutegemea kushinda. Lakini inapotokea ameshindwa, hulalamika au kuona kuwa kaonewa. Anasahau kuwa katika mashindano kuna mshindi na mshindwa. Mara zote mshindi huwa ni mmoja tu....
Mwosha kwa uelewa wangu ni mtu anayetumika kumwosha maiti na kumuandaa kwa mazishi. Zoezi hili la uoshaji hufanywa zaidi na watu wenye imani ya Dini ya Kiislamu. Kazi ya kuosha maiti huwa ni ngumu kidogo ndio maana inafanywa na watu maalumu. Na mwosha huyo naye akifa huoshwa vile vile na mwosha mwingine. Hayo ndiyo maisha yetu sisi wanadamu....
Kuugua ni hali ya kuwa na ugonjwa, na mtu mwenye ugonjwa hujulikana k**a mgonjwa. Mtu anayeugua au mgonjwa hupenda kupata tiba ili aweze kupona. Mara nyingi mgonjwa anapozidiwa, fikra zinazomuujia ni kuwa anaondoka, yaani anakufa....
Hewala ni neno linalomaanisha "ndiyo" au "ni sawa". Hii ina maana ya kukubali na siyo kulazimishwa k**a vile ifanyikavyo kwa watumwa. Mtu anaweza kukubali tu ili wafikie suluhu katika kutokukubaliana kwao au kufikia muafaka kuwa basi na yaishe ili amani tipatikane....
Moshi ni hali ya ukungu wa joto na harufu ya kuunguzwa kwa majani, miti na hata karatasi. Hali hii unaweza kuiona kwa macho pia unaweza kuihisi kupitia kwenye pua. Kwa mfano huwezi kuona moshi unafuka kutoka msituni bila kuwa na moto nyuma yake. Hivyo moto huwa ndiyo sababu ya moshi kufuka....
Mvua ni baraka ambayo huwanufaisha watu wote. Mkulima ama mfugaji akinufaika na mvua, mazao yapatikanayo kutoka kwao yatawanufaisha watu wote....
Matawi ni sehemu ya mti ambayo huchipua katika mti na ile sehemu inayoshika majani. Ni kawaida ya mtu ambaye anapanda au anashuka mtini kushika tawi, asipofanya hivyo anaweza kuanguka....
Watu wengi tunafanya mambo lakini hatuyafanyi kwa bidii, tunafanya ili mradi tu yafanyike. Unaenda kazini lakini huna bidii ya kwenda kazini, leo unaenda kesho hauendi. Kila siku unaenda ukiwa wa mwisho na unatoka ukiwa wa kwanza....
Unaweza ukawa na maumivu fulani k**a ni ya ugonjwa au maumivu mengine ya maisha. Maumivu hayo yanaweza kuwa ni ya muda fulani au kipindi fulani tu lakini mwisho yakapata jawabu. Katika hali hiyo unaweza ukasahau tu pindi pale linapokuja kupata majibu. Hapo itakuwa sio rahisi tena kukumbuka k**a kuna jambo lilikuwa limekutesa. Mfano mzuri ni pale unapokuwa unaumwa lakini ukipona inakuwa sio rahisi tena kukumbuka maumivu uliyokuwa ukipata....
Mara zote unatakiwa kutangaza mema kwa ajili yako. Kila mara jiambie, mimi sio wa kushindwa kwa sababu sikuumbwa kushindwa....
Maji huwa yana nguvu sana yakiwa kwenye njia yake. Pamoja na umuhimu mkubwa wa maji kwa viumbe hai, yakimwagika umuhimu wake unakuwa haupo tena maana huwezi kuyazoa na kuyatumia....
Kupata na kukosa ndio maisha ambayo kila binadamu anapitia kila iitwapo leo. Kusaidiana katika shida na raha ndio kiulimwengu. Hapo ndipo tunapoonyesha upendo wetu kati ya mtu na mtu....
Mwiba ni sehemu ya mti kwenye tawi ambayo lina ncha kali. Usipokuwa makini inaweza ikakuchoma....
OMBA UFAHAMU KATIKA MAISHA YAKO ALFREDA GEORGE Ufahamu ni kujua kipi ni kizuri kwako na kipi ni kizuri kwa jamii inayokuzunguka.Hali kadhalika, ufahamu ni kujua kipi ni kibaya kwako na kipi ni kibaya kwa binadamu wenzio ili uweze kukiepuka. Mtu yeyote mwenye ufahamu hutembea katika haki. Hata k**a kuna jambo baya, atalihukumu katika haki. Katika maisha, inakupasa ujihukumu mwenyewe kwanza pale unapokuwa umekosea. Usisubiri watu wakuhukumu. Watu wengi wana tabia ya kupenda kuhukumu wenzao na sio kujihukumu wenyewe. Hapo ndipo vurugu na kutokuelewana kunapoanzia. Ni kawaida ya wanadamu kupenda kujitetea kwanza. Ukijua kujihukumu katika yale mabaya unayoyatenda, basi utabadilika. Utakuwa mtu wa kuheshimu kila apitae mbele yako. Usipoweza kujihukumu mwenyewe hautakaa ubadilike, zaidi utawachukia wale ambao wanataka ubadilike. Ukweli ni kwamba, ukiwa na tabia hiyo, hautaishia popote zaidi ya kushindwa. Hatua ya kupata ufahamu, huwa ni ngumu sana kuifikia. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kuna vikwazo vingi vya kukutoa katika ufahamu. Hapo ndipo panahitaji uvumilivu maana mambo mengine yatakuudhi na kukukatisha tamaa. Ukibahatika kupata ufahamu, utakuwa umepata kila unachohitaji katika maisha yako. Kwa kawaida, Mungu humtumia mtu mwenye ufahamu na huyo ndiye atakaye sababisha upate kile ambacho umekuwa ukikitamani siku zote. Ili uwe na maisha mazuri, yakupasa uombe kutunukiwa ufahamu na hapo ndipo utakapopata amani....
Maarifa na hekima vina thamani sana kuliko hicho unachokitafuta. Ukiwa na ufahamu na hekima una zaidi ya fedha. Hii ni kwa sababu ukiwa na huo ufahamu na hekima utafanikiwa kuwa tajiri. Hekima itakuongoza kupata kila unachohitaji katika maisha yako....
Kimaisha, binadamu tunapitia pilikapilika mbalimbali. Nyingine ni za furaha na wakati mwingine ni za huzuni zenye kukatisha tamaa....
Ndege ni mkubwa kwa umbile ukimlinganisha na mchwa na sisimizi ndio maana anaweza kuwala wadudu hao bila shida. Lakini ndege huyo huyo akifa biashara inabadika. Akifa anakuwa hana ubabe tena, hivyo mchwa na sisimizi nao wanapata ubavu wa kumla....
Pakacha ni aina ya kapu litumikalo kubebea vitu. Mchukuzi wa kapu hili ni mtu anayebeba mizigo, aidha ikiwa ndani ya pakacha au chombo kingine. Pakacha likijaa vitu linaweza likawa zito lakini jinsi lilivyosukwa linaweza kuruhusu vitu vilivyowekwa humo ndani kuvuja au kumwagika kidogo kidogo wakati vimebebwa na hivyo kupungua kwa uzito ambao humpa ahueni mbebaji /mchukuzi....
Yako mambo yanayotokea katika maisha ya mtu pasipo yeye mwenyewe kujua. Mambo hayo yanaweza yakawa mazuri au mabaya lakini pengine yeye haelewi nini kinaendelea....
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the practice
Website
Address
Bowie, MD
20715
Opening Hours
Monday | 12pm - 8pm |
Tuesday | 12pm - 8pm |
Wednesday | 12pm - 8pm |
Thursday | 12pm - 8pm |
Friday | 12pm - 8pm |
Saturday | 10am - 12pm |
16701 Melford Boulevard
Bowie, 20715
Health and Wellness / Martial Arts / Qigong / Tai Chi Chuan / Mobility
16701 Melford Boulevard, Suite 400
Bowie, 20715
Restore your sense of beauty, balance, and bliss with a personalized holistic strategy to nourish your hair, scalp, mind, body, and spirit.
Bowie, 20720
A hub, in partnership with WellSpring VitalHub, committed to enhancing health and wellness, fitness, optimal nutrition, and preventive health screenings.
Bowie
Bye Bye Belly is the proud home of the Get SNATCHED! Juice We have a variety of products that target weight loss and also offer a wide range of health maintenance products such as...
6710 Laurel Bowie Road #2222
Bowie, 20718
Apryl Showers is a mobile shower and restroom trailer providing a safe, clean environment to perform
Bowie
We offer information on total body wellness and offer products that will help you take your health to an optimum level.
4891 Telsa Drive
Bowie, 20721
RX F.I.T Club (R.O.A.N.E Xperience F.I.T -Faith Ignites Transformation) is a Lifestyle Wellness Trai
17108 Birch Leaf Terrace
Bowie, 20716
I am a multi-faceted, purpose driven health and happiness coach and consultant who is passionate about supporting people in transforming their lives.